Fursa 500 za Ajira kwa Madereva Pikipiki UAE (2026)

Filed in Ajira by on December 29, 2025

Bonyeza KUJIUNGA NASI WHATSAPP Kwa nafasi za kazi, matangazo mbalimbali Ajira mpya kutoka Serikalini, Kampuni, Taasisi mbalimbali TAESA, Viwandani, Internships.

Tangazo la Fursa 500 za Ajira kwa Madereva Pikipiki UAE (2026) maombi yatumwe kwenye mfumo wa

Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano kwa kushirikiana na kampuni ya Target Tours and Labour Supply Company Limited, inawatangazia Watanzania wenye sifa stahiki kutuma maombi ya ajira ya Madereva wa Pikipiki ili kujaza nafasi 500 zilizoidhinishwa na kampuni ya Velo Logistics Delivery Services LLC ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).

Maelezo ya Fursa ya Ajira

KigezoMaelezo
Nafasi ya AjiraDereva wa Pikipiki
TaasisiVelo Logistics Delivery Services LLC
NchiUmoja wa Falme za Kiarabu (UAE)
Idadi ya Nafasi500
UmriMiaka 20 hadi 37

Soma zaidi:

Sifa za Mwombaji

Mwombaji anatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:

  • Awe na elimu ya msingi au sekondari
  • Awe na leseni halali ya udereva wa pikipiki
  • Awe na uzoefu wa kazi wa angalau miaka 2 katika udereva wa pikipiki
  • Awe na hati ya kusafiria (Passport)
  • Awe na uwezo wa kuzungumza na kuandika lugha ya Kiingereza
  • Awe mwanamume

Masharti na Manufaa ya Ajira

  • Mshahara utalipwa kwa kuzingatia Sheria za Kazi za UAE
  • Gharama za matibabu kwa kipindi chote cha ajira zitagharamiwa na mwajiri
  • Tiketi ya kwenda na kurudi itagharamiwa na mwajiri
  • Malazi na chakula vitagharamiwa na mwajiri katika miezi miwili (2) ya mwanzo wa ajira
  • Mwajiri atalipia gharama zote za usafiri wa kutoka nyumbani hadi kituo cha kazi katika miezi miwili ya mwanzo

Aina ya Ajira

  • Mkataba wa ajira wa miaka miwili, unaoweza kuhuishwa

Daraja la Leseni

  • Daraja A, A1 au A3

Ratiba ya Usaili

Dar es Salaam

19, 20 na 21 Januari, 2026
Lumumba, Kariakoo – Jengo la Tahmeed (Ghorofa ya 2)

Mwanza

22, 23 na 24 Januari, 2026
Jengo la Exim Bank (Ghorofa ya 3)

Tanga

26, 27 na 28 Januari, 2026
Jengo la Anjuman

Jinsi ya Kutuma Maombi

Bonyeza hapa kudownload PDF ya tangazo

Waombaji wote wanatakiwa:

  1. Kutuma Wasifu (CV) zao kupitia:
  2. Baada ya kutuma maombi, kujisajili kwenye mfumo wa ajira wa Serikali kupitia: https://jobs.kazi.go.tz

Tags: ,

Comments are closed.